Kuna watu wengi maarufu ambao pesa zao nyingi hupeleka kwenye bata na mambo mengine, lakini kiungo wa timu ya taifa ya Ghana sulley Muntari yeye amewaonea huruma watoto wa mtaani wa brazil kuamua kuwapa neema
Kiungo huyo wa AC millan ambaye yupo nchini brazil na timu yake ya taifa ya Ghana alipewa ruhusa na kocha mkuu wa nchi hiyo Kwesi Appiah kukamilisha azma yake ya kukutana na watu wa kawaida nchini Brazil.
Wakati akitembea mtaani katika mji wa Maceio, tmji ambao timu ya taifa ya Ghana imeweka kambi Muntari alisign autographs na kupiga picha na watu wa kawaida ,napia aliingia mfukoni kuwapa pesa watu wasio jiweza.
Muntari hato cheza mechi inayofuatia dhidi ya Ureno baada ya kupata kadi mbili za njano katika mchozo dhidi ya Ujerumani.
No comments:
Post a Comment